KIDATO CHA 3 $ 4-KISWAHILI-UCHAMBUZI WA TAMTHILIYA

UHAKIKI WA KAZI ZA FASIHI ANDISHI
TAMTHILIYA YA KILIO CHETU
MTUNZI: MEDICAL AID FOUNDATION
WACHAPISHAJI: TPH
CHAPA YA 1: 1996

UTANGULIZI
KILIO CHETU ni tamthiliya inayojaribu kuvunja ukimya uliotawala miongoni mwa wanajamiii katika kutatua matatizo mbali mbali yanayotokana na mahusiano ya kijinsia,matatizo ambayo yasipopata ufumbuzi thabiti yanaweza kuliangamiza taifa.

MAUDHUI : DHAMIRA
(i). ELIMU YA JINSIA
Hii ni dhamira ambayo imetawala katika tamthiliya hii ambapo  wazazi na walezi wengi inaonesha wako tayari kuvunja ukimya uliopo kati yao na watoto wao na kuzungumza waziwazi juu ya mahusiano ya kijinsia.Baba na Mama Anna na mjomba wahusika hawa wamejitoa mhanga ili kuwanusuru watoto wanaoathirika na ugonjwa hatari wa UKIMWI kwa sababu ya kukosa elimu.
Baba na mama Anna wanapeana majukumu ya kuongea na watoto (baba na watoto wa kiume na mama na watoto wakike) kama uk 10 unavyoeleza. “Baba Anna:hili ndilo nimefaulu mwenzenu Nimekwambia,Mama Anna akae na mabinti zake”.Kwa upande mwingine kuna wazazi na walezi ambao wanaamini kuwa kuwaeleza watoto ni kuvunja mila na desturi pia ni kuwafundisha umalaya.Mama Suzi na baba Joti wanawasilisha kundi hili wao wanaamini kuwa viboko na vitisho ndio njia sahihi ya kuwafunza watoto tabia njema.
Matokeo ya misimamo yote miwili imeonekana bayana kwenye tamthiliya hii ambapo,watoto waliopata elimu mfano Anna wanajieleza na wana majibu sahihi kuhusu mahusiano ya jinsia na wale wasio na elimu mfano Joti na Suzi wanapata maradhi mfano Joti alipata Ugonjwa wa UKIMWI na Suzi anapata mimba.kutokana na hali hii elimu ya jinsia ni jambo muhimu sana kwa maisha ya jamii ya sasa,kuendeleza mila kuna liangamiza taifa letu
(ii) MAPENZI KATIKA UMRI MDOGO
Mwandishi ameonyesha jinsi vijana wanavyoshiriki mapenzi katika umri mdogo,jambo hili ni hatari katika maisha yao.Matokeo ya jambo hili ni kupata mimba za utotoni na maambukizi ya virusi vya UKIMWI.Msanii amewatumia wahusika Joti na Suzi kama waathirika na mapenzi katika umri mdogo.Aidha ameonyesha pia tabia ya vijana wadogo kushiriki ngono na watu waliowazidi umri,hali hii pia inazidi kuwaingiza kwenye hatari ya kupata magonjwa.Joti ana mahusiano ya kimapenzi na chausiku (mtu mzima)ambae pia ana mpenzi wake mpemba(uk 23)
Suala la mapenzi katika umri mdogo (kujamiiana) linachangiwa na kuzagaa kwa picha za X na picha za utupu zilizozagaa mitaani(kwenye magazeti,mitandao nk).Vijana na watoto wengi hupenda kuangalia vitu hivyo na kujikuta wakishawishika kufanya ngono .
 (iii)MALEZI
Suala la malezi limezungumziwa katika mitazamo tofauti tofauti ambapo kuna wanaoamini kuwa malezi ya watoto ni kuwapiga viboko na kuwatisha,mwandishi amewatumia mama Suzi na baba Joti ambao wanaamini kuwa viboko vinaweza kuwaadabisha watoto wao, matokeo ya mtazamo huu ni watoto kuwa na nidhamu ya woga na kushindwa kuyakabiri majaribu mfano Suzi anashindwa kumkatalia Joti kufanya ngono na matokeo yake anapata mimba
Aidha kuna wazazi ambao wanaamini malezi bora kwa watoto ni kuwaelimisha na kuwapa mifano halisi ya maisha badala ya kuwatisha,Mjomba,baba na mama Anna wanaamini mfano huu.Anna ameelimishwa na kuelimika hakuna anayemdanganya mfano anamweleza Mwarami kuwa kwa sasa wanatakiwa kuzingatia masomo na si vinginevyo.
Aidha anamweleza Mwarami madhara ya ngono katika umri mdogo pia ni pamoja na kupata magonjwa kama kaswende,kisonono na UKIMWI hivyo wasiogope mimba tu kama walivyodanganyana wao kwa kupeana vidonge vya kuzuia mimba .
Hivyo suala la malezi litazamwe kama jukumu la jamii nzima na kila mwanajamii aone kuwa ana wajibu wa kushiriki malezi.
(IV)  UKIMWI NA TIBA YAKE
Mpaka sasa hakuna tiba kamili ya UKIMWI ambayo imethibitishwa kinachotolewa mpaka sasa ni dawa za kupunguza makali ya virusi vya UKIMWI pamoja na magonjwa nyemelezi (ARV).Dawa hizi hutolewa kwenye vituo vya afya vilivyoidhinishwa na serikali au mamlaka husika.Pamoja na hayo kumekuwapo na matangazo kadha wa kadha kwenye magazeti, runinga au mabango yanayoeleza kuwepo kwa watu wanaodai kutibu UKIMWI, ukweli utabaki kuwa hakuna tiba kama mwandishi alivyoeleza (uk 34), ugonjwa huu hauna tiba ushahidi upo wazi kwani kadri tunavyoona watu walioupata ugonjwa huu, tunajua ukweli kwa hiyo matangazo yanayotolewa mengi hulenga kutuongezea matatizo na pengine kuleta uhasama miongoni mwetu.

(V) NAFASI YA MWANAMKE
katika jamii zetu za kiafrika mwanamke hutazamwa katika sura tofauti mathalani katika tamthiliya hii mwanamke ameonyeshwa katika sura tofautin kama ifuatavyo;
 Mosi,malaya,mtazamo huu umethihirishwa na chausiku ambaye licha ya kuhusiana kimapenzi na joti alikuwa na mpenzi mwingine. (mpemba muuza duka).Suzi naye licha ya kuwa mwanafunzi wa shule ya msingi alijihusisha na uzinzi.
 Pili,Mnyonge hana sauti,mwanamke pia ameonyeshwa kama mtu duni na asiyefaa,asiye na sauti ya kutetea haki zake zote.Mfano mama joti baada ya kubaini mume wake kutokuwa mwaminifu anashindwa kumuuliza badala yake ananunua khanga kuwasema wabaya wake.
Tatu,Mlezi wa familia,mwandishi ameonyesha kuwa mwanamke ni mtu muhimu sana katika malezi mfano,mama suzi yuko mstari wa mbele kumlea mwanawe suzi na kuhakikisha anafuata njia njema impasayo mtoto mwema. Mama Anna naye ameonyesha kumlea vema bintiye Anna na kumwezesha ashinde vishawishi toka kwenye jamii inayomzunguka.
Nne,Mwenye msimamo thabiti,mwanamke pia ameonekana kuwa mwenye msimamo katika maamuzi yake,Mfano Anna anapotongozwa na mwarami anajibu kwa ujasiri kuwa wao bado ni wanafunzi wazingatie masomo anasikika akisema “ya nini kukimbilia suti na nepi hujavaa”.
Tano,mshauri,katika tamthiliya hii mwanamke ameoneshwa kama mshauri bora,mfano Anna anamshauri suzi kutotoa mimba bali amueleze mama yake kuhusu swala hilo.
(VI) MAPENZI NA NDOA
Mwandishi ameonyesha kutokuwepo kwa uaminifu katika suala la mapenzi na ndoa kwa ujumla.Baba Joti ameoneshwa kuwa na wanawake wengi.Joti na Chausiku wana wapenzi zaidi ya mmoja hali inayohatarisha maisha yao hasa kipindi hiki cha ukimwi hivyo uaminifu ni muhimu sana katika mapenzi.
MIGOGORO
Katika tamthiliya hii kuna migogoro mbalimbali imejitokeza ambayo ni;
Mosi,mgogoro kati ya Suzi na mama yake,Chanzo cha mgogoro huu ni vidonge vya kuzuia mimba kwenye sketi yake ya shule jambo ambalo mama yake hakiliafiki na suuhisho ni mama suzi kumwadhibu Suzi.
  Pili,mgogoro kati ya mama Suzi na mjomba,Chanzo cha mgogoro huu ni tofauti za mtazamo kuhusu elimu ya jinsia,mama Suzi aliamini kuwa kumwelimisha Suzi kuhusu mahusiano ya kimapenzi ni kumfundisha umalaya,mjomba anapingana na hilo kwa kumwambia mama Suzi viboko havisaidii
  Tatu,mgogoro kati ya Joti na Chausiku,Chanzo cha mgogoro huu ni tabia ya Joti kuwa na wasichana wengi na kutumia vitu vya Chausiku kuwahonga wasichana wengine,suluhisho ni Chausiku kumkalipia joti.
  Nne,mgogoro kati Mwarami na rafiki zake,(Chogo,Joti na Jumbe) wanamlaumu Mwarami kutochangamka na kuwa na mpenzi wanamwambia kama hachangamki watamtoa umemba.Kauli hiyo ilimfanya Mwarami amfuate Anna na kumtaka kimapenzi.
  Tano,mgogoro kati ya Anna na Mwarami,Chanzo cha mgogoro huu ni tofauti za misimamo,Mwarami anataka Anna akubali kufanya ngono,Anna anakataa na kumweleza kuwa wasome kwanza mambo ya ngono yana muda wake.
 UJUMBE
Ø  Si busara kuchanganya mapenzi na masomo kwani kufanya hivyo huleta madhara(Suzi alipata mimba ,Joti alipata UKIMWI)
Ø  Elimu ya jinsia ni haki na stahiki si halali kwa watoto (vijana) kuwanyima elimu hiyo kwani kufanya hivyo ni kuwaangamiza
Ø  Wazazi wabadilike kulingana na wakati wasing’ang’anie mila ambazo haziisaidii jamii.
Ø  Elimu stahiki kuhusu UKIMWI itolewe kwa wanajamii wote ili wasihusishe UKIMWI na mambo ya kishirikina.
Ø  Wazazi wavunje ukimya na wao bayana kuhusu mabadiliko ya miili yao ili iwe rahisi kushinda majaribu mbalimbali
FALSAFA
Mwandishini anaamini kuwa kuwapa watoto elimu ya jinsia ni kuwafanya wajitambue na kujielewa barabara na kuepuka madhara ya kujiingiza kwenye ngono katika umri mdogo.Elimu ndio njia pekee ya kuwaepusha dhidi ya VVU/UKIMWI.

FANI
   MUUNDO
Mwandishi wa tamthilia ya KILIO CHETU ametumia muundo wa moja kwa moja (msago),mchezo unaanza sehemu ya kwanza ambapo dubwana linaingia kisiwani.
Ø  Sehemu ya pili na ya tatu tunajulisha kifo cha fausta na Suzi kujihusishwa katika mapenzi na kukutwa na vidonge vya kuzuia mimba.Na katika sehemu hii mjomba anawaeleza wazazi wa Suzi na Joti elimu ya jinsia kwa vijana.
Ø  Sehemu ya nne watoto wanajihusisha ngono na wasichana wanaowazidi umri kama Chausiku Aidha mtoto Anna anaonyesha jinsi alivyopatiwa elimu kuhusu jinsia hivyo kushindwa vishawishi
Ø  Sehemu ya mwisho Suzi anagundulika kuwa ana ujauzito wa Joti ambaye amedhihirika kuwa ana ugonjwa wa UKIMWI
MTINDO
Mwandishi ametumia baadhi ya vipengele vya sanaa za maonyesho ya kiafrika.
Mfano;
Ø  Matumizi ya nyimbo (uk 21 na 25)
           Kiongozi; tunaangamia x4
           Wote;tunakwishwax2
    (wanainuka huku wanaendelea na wimbo)
Ø  Pia mwandishi anatumia mwanzo na mwisho wa hadithi ambao ni mwanzo wa hadithi za fasihi simuluzi mfano ‘Paukwa........pakawa
Mtambaji:niendelee nisiendelee
            Wote: endelea
Ø  Mwandishi pia ametumia mtindo wa monolojia pale mtambaji anapotoa maneno ya utangulizi kuhusu matendo yanayohusika/yanayotokea
Ø  Pia kuna matumizi ya dayalojia yenye maneno machache lakini yaliyopangwa kwa ufundi na ustadi mkubwa .
MATUMIZI YA LUGHA
Mwandishi anaonyesha ustadi mkubwa katika matumizi ya lugha inayofanya wasomaji watafakari kwa makini ametumia lugha nyepesi inayoeleweka kwa walengwa(watu wa kawaida) ambao ni watoto na wazazi(walezi).Lugha iliyosheheni tamathali za semi ,misemo nahau matumizi ya lugha za kiingereza na lugha ya kiasili(kibantu)na pia matumizi ya taswira
TAMATHALI ZA SEMI
Tashbiha
·         Walipukutika kama majani(UK 1)
·         Miti inayoungua kama mabua(UK 6)
·         Mbona unakuwa mgumu kama mpingo(uk 5)
·         Unakuwa nyuma nyuma kama koti
Sitiara
·         Ndio mwisho wa kumvumilia huyu nguru anaechimba ndoa yangu(uk2)
·         Huyu kinyago wako anakimbia nini?(uk 20)
Tashihisi
·         Huyu kinyago anakimbia (uk 20)
TANAKALI ZA SAUTI
·         Wacha moyo nipute pwi pwi(uk16)
·         Basi vup nikamdaka(uk 16)
Takriri
·         Pigadomo ,piga domo( uk 16)
·         Watu watapukutika kama majani ya kiangazi
·         Hodi hidi mwenye nyumba (uk 13)
Misemo
·         Na wewe utakuwa nyuma kama koti (uk 4)
·         Mtakatifu wa usoni (uk 9)
·         Mapenzi ni tiba (uk 22)
·         Kukimbilia suti na hali nepi hujavaa (uk 20)
·         Kukausha (uk 9)
·         Anadunda (Uk 8)
·         Umekula wa chuya (Uk 25)
·         Makapera kibao (Uk 7)
·         Kujikaza kisabuni (Uk 21)
·         Kushika hatamu (Uk 22)
Methali
·         Wembamba wa reli treni inapita (Uk 6)
·         Shukrani ya punda ni mateke
·         Asiyefundwa na mamaye hufundwa ulimwengu (Uk 30)
Nahau
·         Kufa kwa kukanyaga miwaya (Uk 9)

LUGHA YA KIINGEREZA NA LUGHA YA ASILI
Kwa kiasi kidogo mwandishi anachanganya lugha ya kiingereza na Kiswahili kutambulisha namna ya vijana wengi wa siku hizi wanavyoongea kwa kuchanganya lugha. Mfano
JOTI;Ndio umecome sio?,maneno mengine ni
·         Stori (uk 16)
·         Umemba(Uk 24)
·         Gest(Uk18)
·         Chips(Uk16)
·         Tuition(Uk 21)
·         Mabuku(Uk1)
Ø  Mwandishi ametumia lugha ya asili katika wimbo wa maombolezo
·         Kiongozi:Jiti afitwe sanda salauyax3
·         Wote:Ena,ena,ena salauya
·         Kiongozi :umwana afitwe sanda x3
·         Wote :ena,ena,ena salauyax3
UTEUZI WA TASWIRA
Mwandishi ametumia taswira la dubwana lililoleta balaa kisiwani (Uk 1)mwandishi anasema kila aliyegusa wakaharisha mara nywele kunyonyoka na vifo vikafuataHaya ni maelezo yanayofanya msomaji ajenge woga na kupata picha halisi ya dubwana yaani UKIMWI

MANDHARI
Mwandishi ametumia mandhari ya mjini hii imedhihirika pale jirani aliposema ‘mie toka siku ile niwaone pale shamba sijakaa tena mjini,nilienda zangu shamba kupambana na nyani wala nafaka’
Pia sinema za x zinadhihirisha mandhari ya mjini
Jumbe:leo si ndio picha
Choggo:ndio tulisahau(Uk 7)
Pia Anna anapoimba (Uk 20)anasema’ pesa zenu,lifti zenu niache mie’wimbo huo umedhihirisha mandhari ya mjini kwani lifti kwa wakina dada hasa wanafunzi zinapatikana mjini kuliko vijijini.

WAHUSIKA
        MAMA SUZI
·         Ni mhusika mkuu msaidizi
·         Mama yake suzi
·         Ana msimamo wa kizamani kuwa mzazi hawezi kuongea na mwanae maswala ya kujamiiana au elimu ya kijinsia haamini kuwa watoto wadogo wanaweza kujihusisha na mapenzi
Mfano Fausta alikuwa mtoto mdogo wa darasa la tano mambo hayo asingeyajua anaamini kuwa njia pekee ya kumfunza mtoto ni kumuadhibu
   SUZI
·         Ni mhusika mkuu
·         Ni mtoto wa mama Suzi,
·         Ni binti mdogo wa darasa la sita aliyejihusisha kimapenzi na Joti kinyume na matarajio ya mama yake.
·         Alikutwa na vidonge vya kuzuia mimba,
·         Hakupatiwa elimu ya kijinsia na wazazi wake,
·         Anapata mimba kutokana na wepesi wa kushawishika
BABA JOTI
·         Ni jirani yake mama Suzi bado ameshikiria ukale kwamba wazazi hawawezi kukaa na watoto wao kuwaeleza habari za ngono anaamini kuwa dawa pekee ya kuthibiti ni viboko na mijeledi (Uk 21)sio mwaminifu katika ndoa yake kwani ana mwanamke mwingine nje ya ndoa
MAMA JOTI
·         Ni mke wa baba Joti
·         Anaamini kuwa watoto wangejua makubwa kwa kutumia methali ‘wembamba wa reli treni inapita (Uk 6).
·         Ndoa yake matatani kwa kuingiliwa na nyumba ndogo .anafikiri suluhisho la tatizo ni kununua kanga za mafumbo
MJOMBA
·         Kaka yake na mama Suzi
·         Ana uelewa mpana na upeo wa kufahamu mambo ya ulimwengu wa sasa ulivyo hivyo anashauri watoto wapatiwe elimu ya jinsia hawatajihusisha na mambo ya kujamiiana mhusika huyu anafaa kuigwa na jamii
BABA ANNA
·         Ni jirani yake na baba Joti
·         Pia ana upeo wa kuelewa mambo na  anamwambia mkewe (mama Anna)akae na watoto wao na kuwaelimisha kufamya mapenzi katika umri mdogo.
·         Anaamini wapo watoto wataelimishwa kamwe hawatajihusisha na kujamiiana
JIRANI
·         Ni jirani yake na baba Joti,
·         Hana uhakika na vipimo vya hospitali anashauri Joti apelekwe kwa fundi(waganga wa jadi) kwa tiba.
·         Anawakilisha watu wengi ambao hawaamini kuwa kuna UKIMWI na mtu akiupata ni kwamba amerogwa.
·         Hafai kuigwa katika jamii
ANNA
·         Ni msichana mdogo ambaye bado ni mwanafunzi amepata elimu ya jinsia na wazazi wake.
·         Huyu ana msimamo na maamuzi ya haraka kuhusiana na maswala ya kujamiiana mfano Uk21......hujui kama kuna madhara mengine....hujui kisonono na mengine kedekede
·         Kutokana na elimu ya jinsia aliyopewa kuepukana na kushinda vishawishi vingi.
·         Pia ni mshauri mzuri, alimshauri suzi asitoe mimba kwani ni hatari (uk 20)
·          Anafaa kuigwa katika jamii
JOTI
·         Ni mwanafunzi wa shule ya msingi anasoma darasa moja na Suzi,
·         Ana uhusiano wa kimapenzi na wasichana wengi akiwemo Suzi,Chausiku,Yoranda,Gelda na sikujua ,
·         Alipata UKIMWI kwa sababu wazazi wake hawakumpatia elimu ya jinsia yaathari za kujamiiana

JINA LA KITABU
Jina la kitabu KILIO CHETU  linasadifu maudhui yaliyomo ndani ,mwandishi ameonyesha kilio cha watoto wakiwalaumu wazazi na walezi wao kwa kutowapatia elimu ya jinsia ili waweze kujikinga na janga hili la UKIMWI.Hiki ni kilio cha jamii nzima ‘wimbo huu unathibitisha
Kiongozo:tunaangamiax4
Watu:tunakishax2
Pia wimbo wa maombolezo kutokana na kilio chetu juu ya janga hili la UKIMWI hSWA WATOTO
KIONGOZI:Joti afwite sanda salauyax3
WATU:Ena ena ena salayax3


Share:

No comments:

Post a Comment

ONLINE VISITORS


Labels

Blog Archive

Recent Posts