WATOTO WA MAMANTILIE
Mwandishi –EMMANUELI MBOGO
UTANGULIZI
“WATOTO WA MAMANTILIE” ni riwaya inayochambua kwa kina adha
wanazozipata akina mamantilie.Hawa wakina mama wametapakaa mjini wakifanya
biashara za kuuza vyakula ili kutafuta chochote cha kuweza kutunza familia zao.
Mwandishi anatueleza kuwa
wakina mama hawa wanaishi maisha magumu,watoto wao ambao wangewasaidia hapo
mbeleni hawapati elimu kutokana na kukosa mahitaji muhumu ya shule.Matokeo yake
wanajiingiza kwenye vitendo viovu ikiwa ni pamoja na matumizi ya dawa za
kulevya,wizi na biashara za madawa ya kulevya.
MAUDHUI
DHAMIRA KUU; UMASIKINI
Hili ni suala ambalo
limeongelewa kwa kiasi kikubwa katika riwaya hii,takribani wahusika wote
wameonekana wakiandamwa na umasikini.Kazi zao ni za kijungujiko (ndogo ndogo)kiasi
ambacho hakiwezi kuwapatia kipato cha kumudu maisha yao.
Mfano katika familia ya MAMA NTILIE
,mwandishi anasema maisha hayaendi bila mama ntilie kwenda kufanya biashara
katika genge la Urafiki ,kilichopatikana kinaishia tumboni.
Ni umasikini huu ndio
unawakatili kulwa na doto ,watoto mapacha walioachwa yatima baada ya mama yao
kufariki .Hata hivyo Doto na Dani wanajiingiza katika ujambazi hatimaye
wanapigwa risasi na kufa.
DHAMIRA NDOGONDOGO
1. Suala la Malezi
Mwandishi amejadili suala hili kwa
kuwatumia Musa,Doto,Kulwa,Peter na Zitta anaonyesha umuhimu wa wazazi wote
wawili katika malezi.Mfano Musa na Dani wamelelewa na mama tu bila baba hali
kadhalika kwa Kulwa na Doto ambao hawakuwa na wazazi wote wawili.Hali hii pia
inaonekana kwa akina Peter na Zitta ambao hawakupata malezi ya kutosha kutoka
kwa baba kwani ambapo alikuwa anaondoka asubuhi kwenda kwenye pombe na kurudi
usiku sana jambo ambalo limechangia kutoweza kutoa mahitaji muhimu kwa familia
yake.
2. Ulevi
Mwandishi amemtumia mzee
Lomolomo ambaye alikuwa mlevi wa gongo tangu alipoachishwa kazi kule bandarini.Mzee
huyo alikuwa akinywa pombe bila kufanya kazi yoyote ya kumletea kipato bali
akiamka asubuhi anakwenda kwenye vilabu vya pombe na kurudi usiku akiwa amelewa
.Ulevi wa namna hii huchangia umasikini katika jamii.
3.
Mapenzi
Katika tamthiliya hii mapenzi
yamejitokeza katika pande mbili yaani yale ya kweli na yale ya uongo
v
Mhusika
Peter ambaye alionyesha mapenzi ya kweli kwa Kulwa na
pamoja na misukosuko aliyoipata kutoka kwa dada yake Zitta.Peter anaonekana
hakuwa na msaada .Peter anasema “Tungoje
mama arudi lakini siwezi .....hatuwezi kumfukuza tutamwacha ateseke huko
mitaani”
v
Mamantilie
anaonekana kuwa na mapenzi ya kweli kwa mumewe kwani pamoja na kwamba alikuwa
mlevi wa kupindukia lakini bado aliweza kumfungulia mlango usiku aliporudi na
kumpa chakula
v
Kwa
upande mwingine mzee Lomolomo hakuwa na mapenzi ya kweli kwa mkewe na familia
yote kwa ujumla kwani hakutoa mahitaji yoyote kama baba wa familia bali alijali
pombe tu.
4
. Suala la Elimu
Elimu ni suala la muhimu sana
kwa taifa lolote lile lenye mipango endelevu.Mwandishi anatueleza kwamba Peter
alipenda sana kusoma shule hata baada ya kufukuzwa shule kwa kukosa ada na sare
lakini jitihada hizo ziligonga mwamba na hivyo ndoto zake hazikutimia sababu ya
umasikini.
4. Nafasi ya Mwanamke katika jamii
Katika riwaya hii mwandishi amemchora
mwanamke katika nafasi tofauti tofauti kama ifuatavyo;
v
Mwanamke
amechorwa kama mhimili wa kiuchumi na kijamii katika jamii,mfano mamantiliye
ameonyeshwa akijishughulisha katika biashara ndogondogo kama vile uuzaji wa
vyakula na vinywaji baridi ili kuweza kukidhi mahitaji ya familia yake, mwandishi
anasema kila kukicha mamantilie na Zitta wanachukua maharage,unga sufuria na
kuni hadi kiwanda cha Urafiki kwa ajili ya kazi na kurudi hadi jioni
v
Mwanamke
amechorwa kama mwenye mapenzi ya dhati,mfano mamantilie alimhurumia mumewe
wakati akirudi amelewa pamoja na kwamba mlevi kupindukia lakini alimfungulia
mlango na kumpa chakula.
v
Mwanamke
amechorwa kama mwenye upendo,huruma na roho ya kutoa msaada.Wanawake watatu
wametumiwa na mwandishi kujadili suala hili,mmoja wapo ni Jane rafiki yake na Mama
Kulwa huyu aliwahurumia watoto wa marehemu rafiki yake akawatunza hadi naye
alipofariki.
Mwingine ni kula aliyemhurumia Peter
wakati Doto alipompiga kule kwenye jaa la taka bila sababu.
Pia
Zenabu aliyempa Peter chai na kipande cha mhogo baada ya kuhisi Peter
alikuwa na njaa.
5. Wizi,Ujambazi na Biashara ya
Madawa ya Kulevya
Vitendo hivi vimeonyeshwa na
mwandishi kwa kutumia wahusika Dani,Kulwa na Doto ambao walijiingiza katika wizi
na ujambazi baada ya kukumbwa na umasikini, waliendakuvunja duka la Mhindi
matokeo yake Dani na Doto wanapoteza maisha kwa kupigwa risasi na mlinzi wa
duka hilo.
Kwa upande mwingine Musa baada
ya kufukuzwa shule kwa kukosa ada na sare anaamua kutorudi tena shuleni na
hivyo anajiingiza katika biashara ya madawa ya kulevya tena anamshawishi na
Peter kushirikiana naye hatimaye wanakamatwa na polisi na kuishia jela
MIGOGORO
v
Mgogoro
kati ya Peter na Doto chanzo ni Doto kumpiga Peter na kumfukuza alipokwenda
kutafuta riziki kule jalalani,suluhisho ni Kulwa kumuonyesha kaka yake kwamba
hakufurahishwa na kitendo cha yeye kumpiga na kumfukuza Peter.
v
Mgogoro
kati ya Zita na Kulwa ,chanzo ni Kulwa kwenda kukaa kwa akina Zita na Peter
suluhisho ni Peter kuingilia kati na kumueleza Zita habari za yeye kuhusiana na
Kulwa.
v
Mgogora
wa nafsi,Kulwa ameonyesha akiwa anawaza juu ya maisha yake ya shida na jinsi
alivyokosa mapenzi ya wazazi,hii ni baada ya Kulwa kuwaona watoto wawili wadogo
wakiongozana na mama yao na kila mmoja akieleza anachotaka mama amnunulie
mwandishi anasema Kulwa alifumbua macho moyo wake ukitoa chozi nafsi yake
ikimsimanga na kumuuliza mama yuko wapi?vicheko na tabasamu zao ziko
wapi?alikaa pale kwa muda.
MTAZAMO /FALSAFA
Mwandishi ana mtazamo wa
kiyakinifu,ana upeo mpana wa kuangalia mambo mfano halidhiki na hali walizonazo
wakina mama hapa nchini ambapo wanahangaika usiku na mchana kufanya biashara
ndogondogo ili kutunza familia zao.
UJUMBE
v
Uhalifu
haulipi mema hivyo mtu anayetenda uhalifu hata kama kuna matatizo
yanayomchochea kufanya hivyo mwisho wake hauwezi kuwa mzuri ndivyo ulivyotokea
kwa wahusika Dani,Doto,Peter na Musa wakati Dani na Doto wanapoteza maisha kwa
ujambazi Musa na Peter wanaishia jela
v
Wakina
mamantilie wanakazi kubwa ya kulea familia hivyo jamii lazima iwasaidie kubeba
mzigo huo
v
Ni muhimu wazazi wahusike katika malezi ya
watoto wao
v
Ulevi si kitu kizuri hivyo jamii inayohitaji
maendeleo ni lazima kupiga vita ulevi
FANI
WAHUSIKA
WAHUSIKA WAKUU
Mamantilie(mama zita)



Mzee Lomolomo




Peter






Zita




WAHUSIKA WENGINE
Mwalimu Chikoya
v
Ni
mwalimu mkuu wa shule ya Nkurumla
v
Aliwafukuza
wanafunzi wake wote kwa kukosa ada na sare za shule
Kulwa na Doto
§
Watoto
mapacha ambao hawakumjua baba yao
§
Waliishi
kisutu kwenye banda chakavu(mbavu za mbwa)
§
Wana
bahati mbaya kwani mama yao alifariki wakiwa wadogo
§
Maisha
yao ya dhiki kwani waliishi kwa kutegemea dampo
§
Doto
anajiingiza katika vitendo vya ujambazi na kupoteza maisha kwa kupigwa risasi
§
Kulwa
anakwenda kuishi kwa mamantilie na hata hivyo anaishia jela baada ya kukutwa
nyumbani kwa Musa ambaye alikuwa anfanya biashara ya madawa ya kulevya
Zenabu




Musa
v
Ni
mmoja wa wanajamii waliofukuzwa shule ya msingi Nkurumla kwa kukosa ada na sare
v
Naye
hamjui baba yake amelelewa na mama tu
v
Hapendi
shule kwani anaona inapoteza muda
v
Anamshawishi
Peter aingie kwenye biashara ya madawa ya kulevya mwishowe wanaishia jela
Muundo
riwaya ya mamantilie ina muundo
“rukia”
kwani mwandishi anatuonyesha kisa Fulani kisha anarukia kisa kingine kile cha
kwanza kabla hajakimalizia,mfano katika sura ya tatu mwandishi anatueleza ugeni
wa mjomba aliyeleta taarifa/habari za ugonjwa wa mama yake mamantilie,anatuonyesha
mamantilie anavyoondoka kwenda Matombo kumuona mama yake kisha anarudisha na
kueleza habari za kuzaliwa na kukua kwa Kulwa na Doto
Riwaya hii ina sura tano zenye vijisehemu
vidogovidogo
Mtindo
Mwandishi ametumia nafsi ya
tatu umoja na wingi pia matumizi ya nafsi ya kwanza naya pili katika vipengele
vichache na ametumia dayalojia(UK 86na 87)
Anatumia mtindo wa fasihi
simulizi ambao umetokana na matumizi ya nyimbo,mfano wimbo ulioimbwa na mzee
Lomolomo wakati anarudi kutoka kwenye pombe na wimbo ulioimbwa na watu wa
mdundiko(UK 9)
Mwandishi ametumia mtindo wa
kuchanganya lugha ya kiswahili na kiingereza “empire” “chloroguinea” “those
wine”, “queen Elizabeth”
Matumizi ya Lugha
Tamathali za Semi
Tashibiha
v
.....akamshika
mumewe kwa mko mmoja kama bua (ni maneno ya mwandishi jinsi mamantilie
alivyomshika mumewe)
v
Mate
yenye harufu kali ya gongo yalimtoka mdomoni kama cheche za moto.Mwandishi
anaeleza mate yaliyomtoka Lomolomo mdomoni wakati aliporudi nyumbani akiwa
amelewa
v
Akaanguka
chini kama mgonjwa mamantilie alimwachia mumewe naye akaanguka chini
v
Hizo
nywele zimekuwa kama kinda la ndege
v
Aliona
ile miguu iliyopekupeku yenye ngozi ya mamba
v
Mikono
yake ilifanya kazi kama mashine
v
Baridi
ilipenya ngozini kama msumari
v
Mdomo
wake ulikaa kama bakuli la pombe
v
Mate
yake yalisafiri na kutua kama roketi na kutua kwenye sikio la Peter pale chini
v
Aliinamisha
shingo nayo ikapinda kama tawi la mforosadi
v
Maumivu
makali yalisambaa kama cheche
v
Moyo
ukamerimerima kama donge la barafu
v
Zita
alianguka chini kama gunia
Tashihisi





Takriri
Ø
“Nakuacha,nakuacha
mamantilie alimwambia Lomolomo wakati anamuinua aingie ndani (UK 12)
Ø
“Baba,baba,amka
baba Kulwa alimuita mzee Lomolomo baada ya kuona haamki (UK 91)
Ø
Twende,twende
mamantilie alimwambia mzee Lomolomo wakati aliporudi kwenye pombe akiwa amelewa
Ø
Kukuru,kakara,kukuru,kakara
wakati Zita na Peter wanapigana (UK 61)
Ø
Nivione
,nivione nivione vinafanya kazi gani ?Zita alimwambia Peter alipomuomba pesa za
kumnunulia Kulwa dawa ya vidonda
TANAKALI SAUTI
v
“Fyzoooio”dereva
wa land river alifyonza baada ya kukwarua mkia wa mbwa aliyemuumiza Zita
v
Alikohoa
ukolio,oklio Lomolomo alikohoa wakati mkewe anamsaidia aingie ndani
v
Peter
aliitikia salamu hizo za ukarimu kwa kupiga chafya mbili tatu.tcha,tcha,tcha
v
Paa,paa,paa
bastola ililia wakati Doto na Dani walipopigwa risasi walipokwenda kuiba kwenye
duka la themfula
Nahau
ü
“Kupiga
usingizi”mlinzi Simango alikuwa amelala
Mdokezo
ü
“Una.....una......”
ü
We
maazita.......una......una(Lomolomo alipotaka kuongea na mama Zita)
UJENZI WA TASWIRA
Mwandishi ametumia taswira za
aina mbili
·
Taswira
zinazoonekana
·
Taswira
za hisi
v
Taswira
zinazoonekana zimetumika pale mwandishi pale anapotumia mbwa mweusi mwenye mkia
mweupe aliyemuumiza Zita na kusababisha mauti yake.
v
Pia
hii inasawiri barabara mazingira ya uswahilini ambako mbwa,mifupa na uchafu
mwingi hutupwa ovyoovyo
v
Taswira
hisi ni pale mwandishi anaposema “hatua chache mbele yake sufuria ,vikombe na
vyombo vingine aliona nzi wakirukaruka juu ya vyombo vile vichafu”
Msomaji anaposoma sehemu hii anahisi
kichefuchefu kwani msomaji atapata picha ya mazingira halisi waishio wakina
mamantilie MANDHARI
Mwandishi ametumia mandhari ya
mjini katika jiji la Dar-es-salaam. .Hii inathibitishwa na majina ya maneno
kama Kisutu,Kiwanda cha Urafiki,Manzese,dampo la Tabata
JINA LA KITABU
WATOTO WA MAMANTILIE kama
ilivyo jina la riwaya linasadifu yaliyomo kwani mwandishi amejaribu kueleza
jinsi wazazi hawa wanavyoishi maisha ya shida wao na watoto wao
No comments:
Post a Comment