KIDATO 3 $ 4-KISWAHILI-UCHAMBUZI WA TAMTHILIYA


ORODHA
Mtunzi;  Steve REYNOLDS
Mchapishaji;Macmillan
Chapa ya 1;2006

UTANGULIZI
ORODHA ni miongoni mwa tamthiliya ambazo zinaonyesha namna jamii hususani watoto na vijana wanavyoangamia kutokana na UKIMWI.Vijana wengi wanaangamia kwa sababu ya ukosefu wa elimu sahihi kuhusu UKIMWI hali hii yaweza kusababisha ongezeko la waathirika,Binti mdogo furaha kwa kutokujua athari za UKIMWI anajiingiza kwenye vitendo vya ulevi na uzinzi kama alivyoshauriwa na rafiki yake Marry na kujikuta akipata UKIMWI mapema hivyo ni vyema asasi kama za dini zihusike katika kutoa elimu hiyo

MAUDHUI
          DHAMIRAKUU : MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI
Mwandishi wa tamthiliya hii amezungumzia kwa kina suala la ugonjwa wa UKIMWI haswa kwa mazingira ya vijijini,mwandishi amebainisha kuwa chanzo kikubwa cha maambukizi ya UKIMWI ni umasikini na ukosefu wa elimu sahihi kuhusu VVU/UKIMWI.Pia mmomonyoko wa maadili,kukosekana kwa uadilifu, ukimya/kukosekana kwa uwazi na hata upendo wa kweli.
   Mwandishi licha ya kuzungumza mambo haya kuwa chanzo cha UKIMWI,ameonyesha mambo ambayo kama yatazingatiwa na jamii inaweza kujiepusha na janga hili la UKIMWI,mambo hayo ni kama ngono salama,uadilifu,elimu,uamiifu,ukweli,upendo,uelewa na uwazi.Kwa ufupi ni kwamba  endapo jamii itazingatia hayo UKIMWI utakwisha, pamoja na dhamira hiyo kuu ya mapambano dhidi ya UKIMWI ,dhamira nyingine ni :-

1 KUKOSEKANA KWA ELIMU
Ujinga humfanya mtu akose maarifa ya kupambana na maisha.Mwandishi wa tamthiliya hii ameonyesha kuwa ujinga na ukosefu wa elimu ya VVU/UKIMWI ni kikwazo cha mapambano dhidi ya ugonjwa huu,elimu hii itolewe kwa watu wa vijijini yaani wajue UKIMWI ni nini,unaenezwa vipi ,unaweza kuepukwa vipi,huduma kwa wagonjwa iweje na je tiba ipo?
  Mwandishi ameonyesha kuwa kwenye kijiji anachoishi binti Furaha hajui UKIMWI ni nini,rejea na mazungumzo ya wahusika hawa;

Mwanakijiji wa kwanza :Ndio lakini kwenye ofisi ya daktari kaambiwa       anaugonjwa wa AIDS
Mwanakijiji wa 4:hicho si kitu kizuri
Mwanakijiji wa 1:wanauita slimu kwa sababu ugonjwa wenyewe unakondesha
Mwanakijiji wa 3:lakini unawezaje kupata ugonjwa kama huo?
Mwanakijiji wa 1:nahisi kuna mtu kamroga pengine rafiki msichana mwenye wivu
Mwanakijiji wa 2:nasikia unapata kwa kugusana tu
Mwanakijiji wa 4:au hata kwa kuwa nao chumba kimoja

2  . UMASIKINI
Umasikini ni hali ya jamii kukosa mahitaji muhimu katika tamthiliya hii umasikini umeonyeshwa kama sababu ya wasichana kujiingiza kwenye vitendo vya ulevi na akina bwana Ecko ili wapate vitu vizuri kama vile viatu,magauni na begi.Umasikini humfanya mtu ashindwe kufanya maamuzi ya busara.Ili kufanikisha zoezi la kupambana na UKIMWI ni vema kwanza wanakijiji wakawezeshwa kiuchumi. Mwanandishi ameonyesha kuwa mwanakijiji akikombolewa kiuchumi atashiriki vema kupambana na UKIMWI

3  .MMOMONYOKO WA MAADILI
Mwandishi wa tamthiliya hii ameonyesha namna jamii inachangia maambukizi ya VVU/UKIMWI
Mfano:furaha na Marry wanatoroka usiku na kwenda kwenye ulevi (baa) na hata kujihusisha katika vitendo vya uzinzi kama kauli ya baba yake anavyodhihirisha “anilichokuwa nafahamu....na hadi sasa Furaha .......ni kwamba amekuwa akitoroka nyumbani usiku wa manane ......kutoroka bila ruhusa .....baa .... ‘wanaume” “wewe”..... “Malaya”....asiye na shukrani’’
Mmomonyoko wa maadili pia umedhihirishwa kwa watu wazima ambao wamekabidhiwa majukumu muhimu katika jamii kama Padri James ni miongoni mwa watu waliopoteza mwelekeo na kujiingiza katika uzinzi na waumini wakeHoja hii imedhihirishwa na padri James mwenyewe anasema “Furaha alikuja kama alivyoagizwa na .....ee.....Ekaristi takatifu ilipatikana,lazima  uelewi jinsi ilivyo vigumu kwa mtu wa hadhi yangu na wadhifu wangu.......?
  Kwa ufupi ni kwamba bwana Ecko,Juma,Kitunda na Padri James ni watu waliotakiwa kuwasaidia wakina Marry na Furaha kufuata mwenendo mwema kwa kuwa kiumri walistahili kuwa baba zao lakini ndio wana uhusiano wa kimapenzi
4 . MAPENZI
  Mapenzi kwenye tamthiliya hii yameonyeshwa kwa namna mbili; Kwanza,mapenzi ya ulaghai baina ya wanandoa na wanajamii kwa ujumla.Mapenzi haya ni yamekwamisha mapambano na mafanikio dhidi ya UKIMWI .
Pili,mapenzi ya ulahai baina ya wanandoa ambapo Bwana Ecko si mwaminifu katika ndoa yake na wanawake wengine wa kijiji chao wana wanaume wengi hali hii inaweka kijiji chao katika hatari ya maambukizi ya VVU/UKIMWI
Juhudi ya kutafuta barua ya orodha ziliwafanya Padri James na wenzake ni ishara ya hofu ya kutambulika kuwa ni waathirika wa UKIMWI kwa sababu walikuwa uhusiano wa kimapenzi na Furaha

5. SUALA LA UWAZI NA UKWELI.
Katika mapambano dhidi ya UKIMWI suala la uwazi ni muhimu sana katika tamthiliya hii.Furaha baada ya kutambua ana maambukizi ya UKIMWI aliamua kuandika barua ya ORODHA kuwataadharisha wanakijiji kuhusu UKIMWI
  Furaha alimwambia mpenzi wake Salim kuwa ana UKIMWI “nina UKIMWI salim’’ zaidi ya hayo,Furaha katika barua yake alitaja mambo ambayo aliamini wanakijiji wakizingatia wataepuka maambukizi ya UKIMWI
Mama Furaha nae alijua bayana sababu ya kifo cha mwanae Furaha kuwa ni UKIMWI.Mama huyu alitambua kuwa ukweli na uwazi ni silaha madhubuti katika mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI
 6.  UKOSEFU WA HUDUMA ZA AFYA
Katika tamthiliya hii mwandishi ameonyesha kuwa ukosefu wa huduma za afya unachangia kwa kiasi kikubwa katika kupoteza maisha ya watu,katika kijiji cha akina Furaha hakukua na huduma za afya ndio maana ililazimu daktari wa Furaha achukue vipimo na kupeleka mjini ambako ndipo huduma hizo zinapatikana ili kubaini tatizo lililokuwa linamsumbua Furaha
  Maisha ya waathirika kama Furaha yalihitaji huduma za afya ziwe bora na karibu na makazi yao.Huduma hizo zitawasaidia kuwapa elimu ya magonjwa kama Malaria pamoja na kifua kikuu
  Pia upatikanaji wa huduma za afya husaidia kuwashirikisha wananchi dhidi ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI
Mwandishi wa tamthiliya hii ameonyesha kuwa suala la ukosefu wa huduma za afya linachangia suala la unyanyapaa kwa wagonjwa wa UKIMWI kuongezeka siku hadi siku na hivyo kuwafanya watu walioathirika wasiwe tayari kujitangaza
 
7.  TIBA YA UKIMWI
Mwandishi wa tamthiliya hii ameonyesha kuwa mpaka sasa hakuna tiba ya kitaalamu ambayo inapatikana,kutokana na hali hiyo watu wengi wamekuwa wakizua tiba mbalimbali mfano imedaiwa kuwa mtu mwenye virusi vya UKIMWI akifanya mapenzi na mtu mwenye bikira hupona kama ilivyoeleza Bwana Ecko
  Ukweli ni kwamba hakuna tiba ya ugonjwa wa UKIMWI kinachotolewa kwa sasa ni dawa za kupunguza makali ya virusi hivyo    na si kutibu
  Kwa mantiki hiyo ni busara kwa jamii kuhakikisha kwamba inaepuka njia zote ambazo zinaweza kusababisha maambukizi ya virusi vya UKIMWI

(B) MIGOGORO
Ni hali ya kutoelewana baina ya pande mbili au zaidi zenye mitazamo tofauti.Katika tamthiliya hii kuna migogoro mbalimbali kama ifuatavyo;
     Mosi,Mgogoro kati ya mama Furaha na Padri James,chanzo cha mgogoro ni Padri James kupinga mama Furaha asisome Orodha hiyo, suluhisho ni mama furaha anamwonyesha kuwa Padri hana cha kuficha hivyo aliisoma hiyo barua kwa nguvu
   Pili,Mgogoro kati ya Furaha na dada mdogo katika harakati za kutoroka usiku kwenda baa,dada mdogo hapendezwi na tabia hiyo na suluhisho ni dada mdogo  kumtisha kwenda kusema kwa mama yao
    Tatu,Mgogoro kati ya baba na Furaha kuhusu kutoroka bila ruhusa ya wazazi na pia kujihusisha na ulevi na umalaya,suluhisho la tatizo hilo ni baba kumpiga mwanae na kumwonya kwa maneno makali
   Nne,Mgogoro kati ya mama Furaha na Salim kuhusu orodha,Salim kutokukubaliana na mama Furaha na kulazimika kuipora orodha na kuichana vipande,suluhisho ni mama Furaha kumkumbusha fadhila za Furaha kwa Salim na kuamua kusoma karatasi iliyobaki na kuokota vipande vile kuviunganisha na kuisoma orodha

 C. UJUMBE
Mwandishi wa tamthiliya hii anatoa ujumbe kwamba;
Ø  Elimu ni silaha muhimu katika mapambano dhidi ya UKIMWI
Ø  Umasikini na ulevi ni vyanzo vingine vya ongezeko la maambukuzi mapya ya VVU/UKIMWI
Ø  Asiyesikia la mkuu huvunjika guu,Furaha hakusikia maonyo ya wazazi wake akapata UKIMWI
Ø  Tamaa mbele mauti nyuma,vijana wengi wanaendekeza tamaa za fedha au vitu matokeo yake ni kupata matatizo mfano Furaha alipata UKIMWI
Ø  Umdhaniaye ndiye kumbe siye,Furaha alikuwa anamwamini Padri James kama mlezi wa kiroho matokeo yake akamwingiza kwenye uzinzi
Ø  Uadilifu,upendo,uaminifu,uwajibikaji na matumizi ya kinga(kondomu) ni baadhi ya mambo yanayoweza kutuepusha na UKIMWI

D. FALSAFA
Mwandishi anaamini kuwa mapambano dhidi ya UKIMWI ni jukumu la watu wote hivyo uadilifu ,uwajibikaji ,upendo,uaminifu ni nyenzo bora katika mapambano hayo

KUFAULU NA KUTOFAULU KWA MWANDISHI
Kimaudhui,Mwandishi amefaulu kufikisha ujumbe wake kwa walegwa.Mwandishi ameweza kujadili vyema tatizo la UKIMWI kwa  kutumia mazingira ya kijijini
Mwandishi ameeleza wasiwasi wake kuhusu uelewa wa watu waishio kijijini kuhusu ugonjwa waUKIMWI lakini pia ameweza kueleza mambo ya msingi ya kuzingatia katika mapambano kwa kutumia mbinu ya waraka (barua ya orodha yenye mambo hayo muhimu ya kuzingatia).Barua ile imetumika kama wosia unasomwa siku ya mazishi siku yenye huzuni na hofu miongoni mwa watu ili kuleta athari za uoga kuhusu UKIMWI
Mwandishi ametumia wahusika wachache ambao hawamchanganyi msomaji.Wahusika wa rika na jinsia mbalimbali wametumika kuwasilisha mawazo ya watu mbalimbali kuhusu UKIMWI kutokana na uzito wa tatizo linalojadiliwa mwandishi amefaulu kutumia lugha inayoeleweka kwa urahisi iliyojaa ucheshi tamathali za semi na mbinu mbalimbali za kisanaa
Vilevile mwandishi amekuwa makini kujadii utamaduni wa jamii husika kwa kutumia tafsida kulinda miiko ya utamaduni wetu katika kutumia lugha
Pia mwandishi amefaulu kupangilia matatizo kutokana na ukubwa wa tukio linalozungumziwa,mwandishi anaanza na msiba kuwa jambo lililopo mbele yetu ni msiba wa jamii na anamaliza na sehemu ya mwisho kwa msiba kuonyesha msisitizo wa dhamira kuu
Kwa ujumla mwandishi amefaulu kwa kimaudhui kufikisha ujumbe kama ilivyokusudiwa kwa jamii

KUTOFAULU KWA MWANDISHI
Mwandishi ameshindwa kuelewa njia mbalimbali zinazoeneza UKIMWI toka mwanzo hadi mwisho wa kitabu mwandishi ameonyesha njia moja tu ambayo ni kufanya mapenzi yasiyo salama
Hii ni muhimu ili kupunguza unyanyapaa.
Mwandishi ameshindwa kugawa kitabu katika maonyesho mbalimbali kitabu kizima kina onyesho moja lenye sehemu ishirini,mwandishi angeweza kuweka shemu katika maonyesho matatu.Hiii ingeweza kufuatilia matukio kwa urahisi zaidi kuliko ilivyo sasa.

FANI
Mwandishi amewagawa wahusika katika makundi mawili yaani wahusika wakuu na wahusika wasaidizi
A.   WAHUSIKA WAKUU
·         Mhusika mkuu katika tamthiliya hii ni Furaha,
·         Msichana aliehitimu darasa la saba,
·         Furaha alijihusisha katika mambo ya uzinzi akiwa na umri mdogo
·         Furaha hakuwa mtiifu kwa wazazi wake kwani licha ya kukatazwa tabia ya utoro wa usiku na ulevi hakuacha tabia hiyo bali aliendelea mpaka alipopata maambukizi ya VVU
·         Hakuwa mwaminifu kwa mpenzi wake Salim,alikuwa muongo kwani alimdanganya Salim hana mwanaume mwingine zaidi yake,
·         Alijihusisha kimapenzi na watu waliomzidi umri ambao sawa na baba yake mfano bwana Ecko na Padri James
·         Alikuwa na tama ya pesa na vitu ,alidanganyika kirahisi mfano Marry alimdanganya kuwa mwema kwa akina bwana Ecko.
·          Si mwaminifu,
·         Muwazi,
·         Mwenye upendo yuko mstari wa mbele kupambana na VVU/UKIMWI
B.   WAHUSIKA WASAIDIZI
Mama Furaha
·         Ni mama mzazi wa Furaha
·         Ni mchapakazi
·         Ni mpole
·         Ni mama mwenye upendo
·         Mkweli
·         Ni muwazi
·         Ana msimamo
·         Anafaa kuigwa na jamii kwani ni mama aliyeejishughulisha  katika ulezi wa watoto na familia nzima
Baba Furaha
·         Ni baba mzazi wa Furaha
·         Ni mkali
·         Ana upendo
·         Ana lugha kali kwa wanae
Marry
·         Ni msichana
·         Ni rafiki yake Furaha
·         Ni Malaya
·         Mlevi
·         Hafai kuigwa na jamii
Bwana Ecko
·         Ni mwanaume mtu mzima
·         Ni mfanya biashara
·         Ni mlevi
·         Hafai kuigwa na jamii,sio mwadilifu katika ndoa yake,ni mwathirika wa UKIMWI
Bwana Juma
·         Ni mwanaume mtu mzima
·         Ni rafiki yake na bwana Ecko
·         Ni mzinzi
·         Ni mtu mwenye tama
·         Ana lugha chafu hafai
·         Hafai kuigwa na jamii
Kitunda
·         Ni kijana wa mtaani
·         Ni rafiki yake na Furaha
·         Ni msanii
·         Sio mwadilifu
·         Sio muwazi
·         Sio mkweli
·         Anaweza kuwa mwathirika wa UKIMWI japokuwa alitumia kondomu baadhi ya siku alizokutana na Furaha
MTINDO
Mwandishi wa tamthiliya hii ametumia mitindo mbalimbali katika kazi yake mfano matumizi ya majibizano (dayaloji) Mtindo huo huruhusu wahusika wake kuzungumza kwa kujibizana mfano mazungumzo kati ya Furaha na Kitunda
Furaha:kuvuta nini lako........(anarudi nyuma)
Kitunda:Mezea mtoto lazima ujifunze lugha za mitaani  

 MUUNDO
Mwandishi wa tamthiliya hii ametumia mtindo wa onyesho ambao sehemu hizo zipo kwenye makundi matatu ambayo yamejipambanua kutokana na matukio mfano sehemu 1-2 ni mazishi ya Furaha ,sehemu ya 3-16 ni makuzi ya maisha ya Furaha kwa ujumla ikihusisha kuugua na kifo chake ,sehemu ya 17-20 ni mwendelezo wa mazishi ya Furaha ikiwemo mchakato wa kutafuta barua ya furaha (orodha)mchakato unaofanywa a Bwana Ecko,Padri James na Salim na mwiso wa mazishi ulioamatana na kusomwa barua ya orodha
MANDHARI
Mwandishi ametumia mandhari ya kijijini.Hii inawakilisha vijiji mbalimbali hapa Tanzania na Bara la Afrika kwa ujumla ,mahala ambapo elimu kuhusu UKIMWI haijaeleweka vema au hakuna kabisa pia huduma za afya kama hospitali hakuna kabisa
MATUMIZI YA LUGHA
Lugha iliyotumika ni ya kawaida inaeleweka na inazingatia maadili ya kitanzania na kueleweka vema kwa walengwa na kwa kiasi fulani tamathali za semi na mbinu nyingine za kisanaa
Misemo/Nahau
Misemo iliyotumika kwenye tamthiliya hii ni kama ifuatavyo ,
v  Shuga dadi”mwandishi akiwa anamaanisha wanaume wenye umri mkubwa wanaopenda kutembea na wasichana wadogo umri sawa na binti zao
v  mshamba “mtu ambae hajui mambo ya mjini au mambo ya kileo
v  furaha anavuna mbegu ya kifo aliyoipanda”kuvuna ni msemo unaomaanisha kupata kitu kutokana na matenyo au maandalizi ,msemo huu ni sawa na “utavuna ulichopanda”
Ø  MISIMU
Mwandishi ameweza kutumia lugha ya misimu ili kuweza kumtambulisha muhusika ,misimu iliyotumika ni ile ya mitaani au ya vijana kutoka kijiweni ,lugha hii tunaweza kuona ikitumika katika mazungumzo kati ya Kitunda na Furaha mfano mshikaji,mchizi ,bomba ,poa majani,nitakulinda ,mwanangu ,kuvinjari haya ni baadhi ya maneno yanayotumika mitaani hususani maneno haya hutumika na vijana wa kijiweni katika mji
Maana ya maneno hayo
Mshikaji-rafiki/jamaa
Bomba mchizi –sawa rafiki/ndugu
Poa-vizuri /sawa
Ganja,majani-bangi
Nitakilinda-nitakusaidia
Mwanangu-mtu wa karibu/rafiki yangu
Kuvinjari-kuzunguka/kutalii
TAMATHALI ZA SEMI
Mfano ....yeye ni kama punda wa kijiji tamathalii hii ilitumiwa kumfananisha Furaha na punda wa kijiji ambae kila mwaname anampenda ,ilitokana na tabia ya Furaha kuwa uhusiano wa kimapenzi na wanaume mbalimbali
Pia Kitunda anafananisha jiji la Dar-es salam sawa na jiji la New york anasema....kisura sawa na jiji la New york
Pia mwandishi anapoonyesha namna vipande vya karatasi vilipoanguka baada ya barua ya orodha kuchanwa na Salim anasema.....vipande vikaanguka kama theruji
Ø  SITIARI
Tamthiliya hii imetumiwa na baba Furaha anapofananisha watoto wake ma mbu wanyonyao damu wasioweza kujitegemea anasema “nyie mbu wadogo
Ø  KIJEMBE
Mwandishi ametumia kejeli kati ya Marry na bwana Juma anasema
Marry:nieleze wewe ni mzee wa kutosha kuwa baba angu
Ø  TAFSIDA
Pia mwandishi ametumia tafsida ili kupunguza ukali wa maneno aliyoyatumia
Mfano :Bwana Ecko:Juma hebu mwangalie yule msichana anavyotingisha kile alichopewa na mama yake
Bwana Juma:kama ulivyofanya wewe mishikaki yangu midogo
Tamathali hiyo(tafsida)imetumiwa badala ya kutaja sehemu zake za siri anazozizungumzia
Ø  TASWIRA
Mwandisha pia ametumia lugha ya picha(taswira)
Mfano,karibu nitakufa njaa hali nyie mbu wadogo mnainyonya damu yangu yote,mbu ni taswira inayoonyesha hali ya utegemezi
JINA LA KITABU
Kitabu hiki kinaitwa ORODHA (The list) neno lenye maana la mfuatano au mfululizo wa vitabu au mambo.Kitabu hiki kinaonyesha orodha zifuatazo
Mosi,Orodha ambayo Furaha alibainisha mambo ambayo yalisababisha kifo chake.mfano;ngono zembe,ukosefu wa elimu,kukosekana kwa uaminifu,umasikini.
 Pili,kuna orodha ambayo ina mambo ambayo jamii inapazwa kujazingatia ili waepuke UKIMWI ambayo ni ngono salama,uadilifu,uaminifu,elimu sahihi kuhusuVVU?UKIMWI
Mwisho,orodha inadhihirika kwa kuitafuta orodha iliyoandikwa na kuachwa na furaha ili isomwe kwenye mazishi yake


Share:

No comments:

Post a Comment

ONLINE VISITORS


Labels

Blog Archive

Recent Posts