Vitate, Vitawe na Visawe

Vitate, Vitawe na Visawe

Baadhi ya maneno ya Kiswahili yanaweza kuwa na maana sawa, maana zaidi ya moja au matamshi yanayotatiza. Vikundi hivi vitatu ni:
  1. Vitate - maneno yanayotatiza kimatamshi. ⇒ '' Vitate hutatiza kimatamshi
  2. Vitawe - maneno yenye maana zaidi ya moja. ⇒ Vitawe hugawanywa kwa matawi au maana zaidi
  3. Visawe - maneno tofauti yenye maana sawa. ⇒ Visawe huwa na maanasawa

Vitate

Maneno yanayotatiza kimatamshi.
  1. ndoa na doa :
    1. ndoa â‡’ kuungana kwa watu wawili na kuishi pamoja kama mume na mke
    2. doa â‡’ alama ya uchafu, kasoro au dosari
    • baba na papa :
    1. baba â‡’ mzazi wa kiume
    2. papa â‡’ mnyama wa baharini
    • fua na vua :
    1. fua â‡’ osha nguo, tengeneza vyuma
    2. vua â‡’ shika samaki kutoka majini; toa nguo
    • faa na vaa :
    1. faa â‡’ inayostahili, inayopaswa
    2. vaa â‡’ weka nguo juu ya mwili
    • ngoma na goma :
    1. ngoma â‡’ ala ya muziki itoayo sauti inapopigwa
    2. goma â‡’ acha kufanya kazi
    • shinda na shida :
    1. shinda â‡’ ongoza katika makabiliano, mashindano
    2. shida â‡’ taabu au matatizo
    • shindano na sindano :
    1. shindano â‡’ makabiliano baina ya watu wawili au zaidi ili kutambua atakayeongoza
    2. sindano â‡’ kifaa kinachotumika kushonea vitu
    • pinga na piga :
    1. pinga â‡’ kutokubaliana na jambo fulani
    2. piga â‡’ kugonga au kuchapa
    • fahali na fahari :
    1. fahali â‡’ ng'ombe wa kiume. pia ndume
    2. fahari â‡’ kujivunia, furaha
    • haba na hapa :
    1. haba â‡’ kisichokuwa kingi
    2. hapa â‡’ mahali karibu
    1. }

    Vitawe

    Mano yenye maana zaidi ya moja
    1. paa :
      1. kwea (enda juu)
      2. mnyama wa porini anayefanana na mbuzi
      3. sehemu ya juu ya nyumba
      • shinda :
      1. kaa au ishi mahali/wakati fulani
      2. ongoza katika shindano
      3. tupu
      • kaa :
      1. sehemu yenye moto ya kuni
      2. mnyama wa majini
      3. keti chini
      4. kuwa mahali fulani kwa muda
      • mbuzi :
      1. mnyama anayefugwa kama ng'ombe
      2. chombo cha kukunia nazi
      • mlango :
      1. ukoo au watu wenye asili smoja
      2. sehemu ya kuingia kwenye nyumba
      3. kitu kinachotumika kifunga nyumba
      • fua :
      1. unda vyombo/vifaa mbalimbali kwa kupiga chuma
      2. osha nguo
      • vua :
      1. toa nguo kutoka mwilini
      2. toa samaki kwenye maji
      • kiboko :
      1. mnyama mkubwa wa baharini
      2. silaha inayotumika kwa kuchapa au kupiga
      • tembo :
      1. aina ya ndovu
      2. aina ya pombe
      1. }

      Visawe

      Maneno tofauti yenye maana sawa.
      1. msichana au banati : ⇒ kijana wa jinsia ya kike
      2. mvulana au ghulamu : ⇒ kijana wa jinsia ya kiume
      3. huzuni au majonzi : ⇒ hali ya kilio na huruma
      4. mazishi au matanga : ⇒ shughuli za kumzika marehemu
      5. wakati au mwia : ⇒ wakati au muda
      6. mtu au mja : ⇒ mnyama atembeaye kwa miguu miwili mwenye uwezo wa kuongea na kufikiri kimantiki
      7. barua au waraka : ⇒ kartasi inayoandikwa na kutumwa ili kuwasilisha ujumbe fulani
      8. siri au faragha : ⇒ jambo lisilopaswa kujulikana na mtu mwengine
      9. macho au maninga : ⇒ sehemu za mwili zinazotumika kuangalia na kuona
      10. mwangaza au nuru : ⇒ miyale inayowezesha watu kuona vitu
      11. Mungu au Mola au Rabana au Jalali au Rabuka : ⇒ Majina ya Mwenyezi Mungu
Share:

ONLINE VISITORS


Labels

Recent Posts